Tony Alexander Adams (alizaliwa 10 Oktoba 1966) ni mchezaji wa zamani wa mpira wa miguu na kocha kutoka Uingereza. Adams alichezea klabu ya Arsenal pamoja na timu ya taifa ya England, na alikuwa nahodha wa timu zote mbili. Alijulikana kama “Mr. Arsenal” kutokana na kutumia maisha yake yote ya soka ya miaka 19 akiwa klabu hiyo kama beki wa kati, akicheza jumla ya mechi 672 na kushinda mataji manne ya ligi ya England. Anachukuliwa kuwa mmoja wa wachezaji bora zaidi kuwahi kuichezea Arsenal[1] na pia ameorodheshwa katika orodha ya Football League 100 Legends.

Marejeo

hariri
  1. [(https://www.arsenal.com/history/gunners-greatest-50-players) "Gunners Greatest 50 Players"]. Arsenal.com. Iliwekwa mnamo 10 Aprili 2023. {{cite web}}: Check |url= value (help)
Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Tony Adams kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.